TCU ITAFUNGUA MFUMO (CAS) KWA SIKU TATU TAREHE 24 HADI JUMATANO TAREHE 26 OKTOBA 2016

on Friday, October 21, 2016


Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania


TAARIFA KWA UMMA

Tume ya vyuo Vikuu (TCU) inautangazia Umma kuwa baada ya kukamilisha mchakato wa maombi ya  waombaji wa vyuo vikuu, vyuo Vikuu Vishiriki na Taasisi za elimu ya juu kwa awamu ya kwanza, ya Pili na ya tatu, na matokeo ya waombaji wote waliofanikiwa kupata nafasi vyuoni kukamilika, Tume ya vyuo Vikuu imebaini kuwa bado kuna waombaji takribani 5,301 ambao bado wako kwenye mfumo na  hawajakamilisha maombi yao.

Tume imebaini pia kuwepo kwa idadi kubwa ya waombaji hasa wenye Stashahada ambao hawakuomba  kabisa kutokana na matokeo yao ya mitihani kuchelewa kufika Baraza za Vyuo Ufundi (NACTE)  

  • Awamu hii itawahusu:
  • Waombaji ambao bado wako ndani ya mfumo ambao hawajapata nafasi
  • Waombaji wapya ambao hawakuwahi kuomba awali; na
  • Waombaji walio na sifa linganifu ambao hawakukamilisha taratibu za uombaji hapo awali

Kutokana na sababu tajwa hapo juu, tume inautangazia Umma kuwa itafungua Mfumo (CAS) kwa siku tatu tu, kuanzia Jumatatu tarehe 24 hadi Jumatano tarehe 26 Oktoba 2016 ili kuruhusu Makundi tajwa hapo juu kuingia kwenye mfumo kutuma maombi.

Waombaji wa awamu ya Nne wanasisitizwa kuzingatia yafuatayo:

  •  Kuhakikisha wanaomba kozi walizo na sifa stahiki
  • Kuhakikisha wanakamilisha maombi yao kiufasaha
  •  kuhakikisha wanajiridhisha na nafasi zilizopo kwa kuzingatia viwango vyao vya ufaulu.

Aidha Tume inapenda kuujulisha Umma kwamba kozi zote zisizo onekana kwenye mfumo kwa sasa kuwa zimejaa.

Baada ya tarehe tajwa hapo juu tume itafunga rasmi zoezi la udahili kwa mwaka2016/17 ili kuruhusu michakato mingine ya Bodi ya Mikopo na Vyuo kuendelea.

Kaimu Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
21/10/206

0 comments:

Post a Comment