CALL_FOR_THIRD_ROUND_OF_APPLICATIONS-2016-17.

on Monday, October 10, 2016


TUME YA VYUO VIKUU TANZANIA TCU
TANGAZO KWA UMMA

Tume ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) inautangazia Umma kuwa imekamilisha kuchakata maombi ya  kujiunga na Vyuo Vikuu na Taasisi za Elimu ya Juu kwa  awamu ya kwanza na ya pili. Orodha na majina ya walichaguliwa  yameshapelekwa vyuoni  kwa ajili ya kuiidhinishwa na Seneti za vyuo husika. Baadhi ya vyuo vimeshaanza kuyatangaza.

Hata hivyo, kuna waombaji ambao bado wako kwenye mfumo na  hawajachaguliwa kwenye kozi yoyote kati ya walizoomba kutokana na sababu  mbalimbali  kama ifuatavyo

Ushindani mkubwa  katika programu za masomo walizoomba ukilinganisha na  ufaulu wao

Waombaji kushindwa kukamilisha taratibu za uombaji; na

Waombaji kutokuwa na sifa kwa kozi walizoziomba.

Kutokana na hali hiyo, Tume inautangazia umma kuwa mfumo wa udahili  utafunguliwa tena kwa awamu ya tatu mnano tarehe 10 mpaka tarehe 16 Oktoba 2016 ili kuruhusu waombaji na aina hii kufanya uchaguzi upya au kukamilisha maombi yao.

Tume inapenda kufafanua  kuwa programu za masomo  zisizoonekana kwenye mtandao zimekwishajaa, hivyo waombaji watalazimika kuomba zile tu  zinazoonekana mtandaoni.

Zoezi hili la uombaji  kwa awamu ya tatu linawahusu waombaji wenye sifa za kidato  cha Sita, Stashahada na sifa linganishi. Hakutakuwa na malipo yoyote kwa waombaji hawa. Tume inapenda kusisitiza kwamba awamu hii haitawahusu  waombaji wapya, ambao hawakuwahi kujisajili wala kuomba udahili kwa awamu ya kwanza na ya pili.

Imetolewa na
Katibu Mtendaji
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
10/10/2016

Source:

http://www.tcu.go.tz/images/documents/CALL_FOR_THIRD_ROUND_OF_APPLICATIONS-2016-17.pdf

0 comments:

Post a Comment